Mapenzi ya mpira wa miguu ni ngumu sana kulinganisha na mapenzi ya vitu vingine hapa kuna watu wananielewa na wapo wasioweza kunielewa...Chukua kama ilivyo!
Kuna siku nimekaa na jamaa yangu mtaani ghafla mpenzi wake akampigia simu, na sio tu mpenzi wake bali ni mpenzi aliyempenda sana na alimpata kwa taabu ... Alimpigia akamwambia kuwa ‘Babe nnatoka mjini sasa hivi nnaomba tuonane nyumbani nnahamu kubwa sana na wewe’!
Bila kusita wala kujiuliza mara mbili jamaa akamjibu kuwa ‘kwasasa haiwezekani ninampango wa kwenda kuangalia mpira nusu fainali ya uefa tutaonana baada ya hapo’! hapa ndipo mapenzi ya mpira yalipozidi mapenzi ya penzi jipya!
Na kupitia hilo pia nliweza kushuhudia mapenzi makubwa ya watanzania kwenye mpira wa miguu katika mechi ya fainali ya kwanza kati ya Yanga dhidi ya USM Algers, ambapo ulipelekea maafa kwa baadhi ya watu kutokana na sababu mbali mbali.
Kwanza ninampongeza Mh.Rais Samia na wadau wengine kwa kuunga mkono hamasa kuelekea mchezo ule kwa kununua tiketi ili watu waweze kufika uwanjani kuwa-support wachezaji katika mchezo muhimu ila ajabu ni kwamba serikali ambao ndio wamiliki wa uwanja wa Benjamin Mkaba pamoja na mamlaka nyingine pia zinazohusika na mpira nchini walifeli kuhudumia kundi kubwa la wapenda soka na kusababisha kifo na watu wengine kupata majeraha (kwa taarifa iliyotolewa na Waziri wa afya)
Kama mdau ninashauri sana wenye mamlaka wa ule uwanja na viwanja vingine watengeneze utaratibu mzuri wa uingiaji pamoja na utokaji uwanjani, ili wengi wavutiwe kufika uwanjani kupata burudani na sio maumivu.
Using hashtags effectively in your Facebook posts can help increase your visibility and at...